Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    KahawatunguKahawatungu
    Button
    • NEWS
    • BUSINESS
    • KNOW YOUR CELEBRITY
    • POLITICS
    • TECHNOLOGY
    • SPORTS
    • HOW-TO
    • WORLD NEWS
    KahawatunguKahawatungu
    EAST AFRICA

    Samaki Tani 11 Kutoka China Wateketezwa Tanzania Kwa Madai Ya Sumu

    Wycliffe NyamasegeBy Wycliffe NyamasegeMarch 14, 2019Updated:March 14, 2019No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter WhatsApp Telegram Email
    samaki wateketezwa tanzania
    Share
    Facebook Twitter WhatsApp Telegram Pinterest Email Copy Link

    Shehena ya samaki wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili (TSh 60 milioni) kutoka China wameteketezwa katika dampo la Pugu Kinyamwezi Jijini Dar Es Salaam, Tanzania kwa madai ya kuwa na sumu.

    Samaki hao ambao wanakisiwa kuwa takribani tani kumi na moja waliteketezwa mnamo siku ya Jumatatu baada ya kubainika kuwa wana madini ya Zebaki.

    Kulingana na Mkurugenzi Msaidizi wa Ulinzi Rasilimali za Uvuvi, Nchama Marwa, madini hayo yana madhara kwa jamii na yana uwezo wa kusababisha Saratani na kuharibu uzazi.

    Zoezi hilo lililosimamiwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh.Luhaga Mpina, liliamrishwa baada ya Wizara yake kushinda kesi iliyokuwa imewasilishwa kupinga hatua iyo.

    Wakishuhudia zoezi hilo, wamiliki wa shehena iyo, wameipongeza serikali kwa hatua hiyo na kuziomba taasisi za serikali kushirikiana ili kuwapunguzia hasara waliyoipata.

    Mpaka sasa, vyombo vya habari kutoka nchi ya Tanzania vimebaini kuwa takriban tani 31 wa samaki wanaoingia nchini kutoka China wameteketezwa.

    Inadaiwa kuwa, serikali imekaza kamba katika ukaguzi huo ili kuhakikisha kuwa samaki wanaoingia nchini ni salama kwa binadamu.

    Aidha, serikali imewaomba wanainchi kuripoti visa vya samaki hatari kama hao kwa vituo vya usalama ili kulinda maisha ya binadamu.

    Soma:Tanzania Yabatilisha Sherehe Za Siku Ya Wanawake Duniani, Yavitaka Vyama Pinzani Kujiunga Na Serikali Katika Maadhimisho Rasmi

    Kando na Tanzania, visa vya samaki kutoka China pia vimeripotiwa nchini Kenya huku raisi Uhuru Kenyatta akikashifu hatua ya kuagiza samaki kutoka nje.

    “Jameni tunatoa samaki kutoka China na wenzetu hapa… hata kama finance bill imepita, tunaweza sema hiyo samaki imeingia ni mbaya, kuna njia nyingi serikali inaezafanya kazi ndo tuhakikishe watu wetu wanafaidika,” Raisi Kenyatta alisema.

    Licha ya madai ya raisi, duru za kuaminika zinaarifu kuwa samaki kutoka China ni wengi nchini.

    Email your news TIPS to Editor@kahawatungu.com or WhatsApp +254707482874. You can also find us on Telegram through www.t.me/kahawatungu

    Email your news TIPS to Editor@Kahawatungu.com — this is our only official communication channel

    Samaki Tanzania
    Follow on Facebook Follow on X (Twitter)
    Share. Facebook Twitter WhatsApp LinkedIn Telegram Email
    Wycliffe Nyamasege

    Email news@localhost

    Related Posts

    Unions back Kenya-US health deal, cite job security

    December 21, 2025

    Man found dead in toilet in Parklands

    December 21, 2025

    One killed, dozens injured at Asake music concert in Nairobi 

    December 21, 2025

    Comments are closed.

    Latest Posts

    Why passport stamps may be a thing of the past

    December 21, 2025

    Unions back Kenya-US health deal, cite job security

    December 21, 2025

    Man found dead in toilet in Parklands

    December 21, 2025

    Gunmen kill 10, wound 10 more in South Africa shooting

    December 21, 2025

    One killed, dozens injured at Asake music concert in Nairobi 

    December 21, 2025

    Al-Shabaab Releases Video of Kenyan UN Worker Pleading for Help

    December 21, 2025

    NPR Officer Arrested, AK-47 Seized in Igembe South Robbery Investigation

    December 21, 2025

    Rachel Ruto Celebrates President William Ruto’s 59th Birthday With Heartfelt Prayer

    December 21, 2025
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest
    © 2025 Kahawatungu.com. Designed by Okii.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.